Posts

Showing posts from May, 2017

JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM ALIHAMISI SOMO HILI NI MBARAKA SANA

Image
Thursday, May 25, 2017 SOMO: SIKU DUNIA ITAKAPOSIMAMA. Mwandaaji: Clinton Omuyanja, Mwenyekiti Msaidizi wa Union  Fungu kuu: Yoshua 10:12,13. Mathayo 27:45-53.  Wimbo namba 107 kitabu kidogo. Je, umewahi  kusikia dunia iliwahi  kusimama.  Wataalamu wa jiografia wanadai kuwa,  dunia inapozunguka katika mhimili wake tunapata usiku na mchana. Dai hili si kweli kwa  kuwa tangu mwanzo Mungu aliumba nuru na giza, nayo nuru ikatawala mchana na giza  usiku [Mwanzo 1:4,5,16]. Ni kweli kuwa dunia imewahi kusimama zaidi ya mara moja katika historia. Dunia  ilisimama wakati Yoshua akikabiliana na majeshi ya wafalme watano waliokwea dhidi  yake na wana wa Israeli. Kwa ajili ya maombi ambayo Yoshua alimwomba Mungu,  Dunia ilisimama kwa kuwa jua liliposimama haukuwa utaratibu wa kawaida kwa dunia. Leo vijana tulioitwa na Kristo tunaitazama  dunia ambayo inaenda kwa mwendo  unaoelezwa na Isaya 24:19 kuwa dunia inayumba yu...

JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM SOMO LA TATU

Image
ENDELEA KUBALIKIWA Wednesday, May 24, 2017 SOMO: UTUME NI WETU SOTE. Mwandaaji: Maregesi January Simula, Mwenyekiti TUCASA SEC 2017/18 Fungu kuu: Mathayo 28:19, 20.  Wimbo namba 107 kitabu kidogo. SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017  TUCASA STUM Baada ya kufa kwa Mwokozi wanafunzi walikata tamaa sana na kufa moyo. Jua la  matumaini katika mioyo yao lilikuwa limekuchwa, na giza ndilo liliwafunika.  Waliyakumbuka maneno ya Kristo wakiwa katika hali ya ukiwa na upweke kabisa.  Maneno ya Kristo yalisema hivi; “Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti  mbichi, itakuwaje katika mkavu?” Luka 23:31 Wanafunzi hali wakijawa na huzuni na majonzi wakiwaza sana kwamba ikiwa Yesu  waliyemwamini na kumtegemea amefanyiwa hivyo wao je, ni nini kitakachowapata  wao? Kwa hofu hiyo walikusanyika katika chumba cha juu, wakafunga milango,  wakiogopa wasipatwe na mambo yaliyompata Yesu. Hapa ndipo Mwokozi alipokutana  nao baada ya kuf...

JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM

Image
SOMO LA PILI  Tuesday, May 23, 2017 SOMO: MTAZAMO, MSIMAMO NA MAONO YATAKAYO BADILI ULIMWENGU KWA WAKATI KAMA HUU. Mwandaaji: Karangi Joel, Mwenyekiti wa TUCASA ETC SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017  TUCASA STUM Fungu kuu: Mwanzo 32:24-26.  Wimbo namba 107 kitabu kidogo. Changamoto za sasa za kimaisha, kielimu, kiuchumi na kijamii wanazokumbana nazo  vijana wakike na wakiume zimekua chachu kubwa kwa vijana kukata tamaa ya maisha  na kurudi nyuma katika maisha yao ya kiroho. Mipango ya maisha ya baadae ambayo  vijana  wamekuwa  wakijiwekea na ndoto ambazo wamekua wakizitazamia zitimie katika  maisha yao zimekuwa  zikipotea pale tu changamoto zinapo wakabili nawao kushindwa  kukabiliananazo. Hali hii imewafanya vijana wengi hasa wanafunzi na wale wasio wanafunzi ambao  wamekutana na nyakati tofauti kama hizi katika maisha kuchukua maamuzi yasiyo  sahihi. Maamuzi hayo yamepelekea  kudumb...

JUMA LA MAOMBI TAR 21/5 LA TUCASA STUM

Mpendwa mtembeleaji wa blogg hii nimekuwekea juma la maombi  Sunday, May 21, 2017 SOMO: ONGOA ROHO MOJA, SHIRIKI KUUBADILISHA ULIMWENGU. Mwandaaji: ESTHER MAYUNGA, MHAZINI MKUU ETC Fungu kuu: Marko 16:15. Wimbo namba 107 kitabu kidogo. Bwana ametuita kuubadilisha ulimwengu kwa kuokoa wengine. Ni kazi ya pekee  ambayo malaika hutamani kuifanya lakini Bwana ameiacha mikononi mwetu kwa ajili ya  ukombozi wa maisha yetu. Mpendwa,  katika mwaka 2017/2018 wa utendaji  umejiaandaaje  kushiriki katika  kuubadilisha ulimwengu kwa kuokoa wengine ambao  hawajamjua Mungu wa pekee na wa kweli. Kwa kutambua kusudi la kuokolewa kwake, mtume Paulo anasema,  “Ya kuwa  sikujiepusha katika kumtangazia neno lolote liwezalo kufaa, bali naliwafundisha  waziwazi na nyumba kwa nyumba [Matendo 20:20]’ Kazi ya  kupeleka Neno  la Mungu  kwa kila mlango wa  mtu na kutafuta  kwa ajili ya Kristo roho zinazoangamia kwa kuk...

INJILI MTANDAONI

MPENDWA MTEMBELEAJI WA BLOG HII KARIBU VIPINDI VYETU VITAANZA HIVO KUANZIA TAR1/6 NAKUENDELA TUTAKUA MUBASHARA KABISA KUKUJUZA HABARI ZA UPENDO WA YESU USIKOSEEE Ev Mwasiposya Y atakua nasi katika IJUE BIBLIA

HAZINA YA PEKEE MAISHANI

Image
SOMO 1;SIRI YA  KAZI SEHEMU YA KWANZA KAZI NI NINI? Ni aina yoyote ya shughuri aifanyayo mtu inayoweza kumpatia cha kutosha kukidhi mahitaji yaketa kipatO MPANGO WA MUNGU WA KAZI MUNGU alikusudia mwanadamu afanye kaz hivyo kazi hivyo ebu tuangalie je kazi imeanza lini katika biblia KABLA YA ANGUKO MWANZO 2:8,15 Kazi ilikusudiwa na mungu kuwa ni mbaraka tunaona kazi aliyopewa aadamu na mungu ni kulima na kutunza bustani ambayo mungu aliianzisha kule edeni hivyo kazi haikuletwa kkwa sababu ya dhami bali ulikua ni mbaraka wa mungu kwa watu wake aliowaweka ktika bustani ya edeni JE BAADA YA ANGUKO KAZI ILIIENDELEA? NDIO HEBU TUSOME MWANZO 3:17 Mungu anasema utakula mazao yako siku zako zot hivyo kwa usahidi huo kazi ilibaki kua mubaraka MWANZO 3:19 Mungu anasema kwa jasho utakula hivyo baada ya anguko magugu na miiba ilihus ishwa hivyo likawepo hitaji la kuongeza juhudi katika kufanya kazimaana adamu aliambiwa kwa jasho lako utakula hivyo mtu anapoacha kuf...
Image
NUKUU ZA AJABU MAMA ELEN G WHITE JUU YA SHETANI NA MBINU ZAKE  CHA KUFANA NI NINI YESU ANASEM,A WITO WETU JIONI HII NI  YATOE MAISHA YAKO KWA YESU AKUONGOZE SALAMA HAKUNA UJANJA

KONA YA INJILI

WIMBO HUU UWE MAALUMU KWAKO MTEMBELEAJI WA MTANDAO HUU NA MUNGU AKUBARIKI 
Image
HATIMAYE TUCASA KANDA YA MOROGORO WAWEKA  WAKFU VIONGOZI WAO Ilikua ni tukio la aina yake lililofanyika katika ukumbi wa Sua mazimbu chini ya viongozi wa kanisa  na wachungaji akiwepo pastor Nkya  na pastor Mika Angalia picha za matukio yot hapa Kwaya ya kanda ikitoa hduma katika kutano hilo kubwa la kipekeeee sana Baada ya ibada vijana wa yesu walipata mda wa kumtafakari MUNGU waooooooo PICHANI NI VIONGOZI WASTAAFU CHINI YA PR NKYA NA DADA  MARIAMU MOTTO imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyetutuma ingali mchanaa picha na BARAKA MUYENGI