JUMA LA MAOMBI TAR 21/5 LA TUCASA STUM

Mpendwa mtembeleaji wa blogg hii nimekuwekea juma la maombi 



Sunday, May 21, 2017SOMO: ONGOA ROHO MOJA, SHIRIKI KUUBADILISHA ULIMWENGU.Mwandaaji: ESTHER MAYUNGA, MHAZINI MKUU ETC

Fungu kuu: Marko 16:15. Wimbo namba 107 kitabu kidogo.
Bwana ametuita kuubadilisha ulimwengu kwa kuokoa wengine. Ni kazi ya pekee 
ambayo malaika hutamani kuifanya lakini Bwana ameiacha mikononi mwetu kwa ajili ya 
ukombozi wa maisha yetu. Mpendwa,  katika mwaka 2017/2018 wa utendaji 
umejiaandaaje  kushiriki katika  kuubadilisha ulimwengu kwa kuokoa wengine ambao 
hawajamjua Mungu wa pekee na wa kweli.
Kwa kutambua kusudi la kuokolewa kwake, mtume Paulo anasema,  “Ya kuwa 
sikujiepusha katika kumtangazia neno lolote liwezalo kufaa, bali naliwafundisha 
waziwazi na nyumba kwa nyumba [Matendo 20:20]’ Kazi ya  kupeleka Neno  la Mungu 
kwa kila mlango wa  mtu na kutafuta  kwa ajili ya Kristo roho zinazoangamia kwa kukosa 
ukweli ni ya muhimu na inahitajika sasa. Katika kipindi hiki ambapo muda si mrefu 
historia ya ulimwengu itafungwa, Bwana ametuagiza wanaume na wanawake, na 
wazee kwa vijana kwenda ulimwenguni na kuihubiri injili kwa kila kiumbe [Marko 16:15].
Kabla na baada ya Yesu kusema, ‘Enendeni’. Aliahidi uwezo, kwanza ‘uwezo wote’ 
kutoka kwenye Kiti cha  enzi. Pili kuwako kwake, hapa mpaka mwisho [Biblia Ya Sema 
uk,97]. ‘Sisi sote tu wajumbe wa KRISTO.  “Maana  Mungu alikuwa ndani ya Kristo 
akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake naye ametia neno la upatanisho ndani yake. 
Baba wa Mbinguni leo anasihi kupitia maisha yetu, tuweze kuupatanisha ulimwengu na 
Mungu kwa ajili ya Kristo [2 Kor 5:19,20].
‘Ujumbe wa  malaika wa tatu ambao ni ujumbe wa kuhesabiwa haki kwa imani katika 
Kristo Yesu, Kristo ni haki yetu. Ni muhimu kiasi gani basi kwa watu wa Mungu 
kujifunza kwa bidii ukweli huu na kuuishi kwa ajili ya wokovu wetu wenyewe na pia kwa 
ajili ya wokovu wa wale  tunaotakiwa  kuwapelekea ukweli huu wa leo. [Ujumbe wa 
Mwisho uk. 161, 162].
Tumeokolewa ili kuokoa wengine. Wale wote walio tayari kutumika kwa kazi ya Bwana 
pasipo kujali udhaifu wao, Bwana atawafundisha jinsi ya kuenenda kwa ujasiri wa 
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017  TUCASA STUM
imani. Atawafanya wawe imara kwa kuunganisha udhaifu wao katika nguvu zake. 
Atawafanya kuwa na hekima kwa kuunganisha kutokujua kwao na hekima yake 
[Mapambano na Faraja sehemu ya kwanza uk 123].’ Leo kama mtaisikia sauti yake 
msifanye migumu mioyo yenu.’
Kupitia utume wa nyumba kwa nyumba, mihadhara ya neno la Mungu, michango, 
maombi na mwenendo safi wa kila mmoja katika kipindi hiki cha ushirikishwaji wa kila 
mwana TUCASA. Tumia muda wako kuubadili ulimwengu kwa Neno la Mungu maana 
BWANA amekuokoa ili uokoe  wengine. Weka mpango wa kuleta angalau roho moja 
kwa Kristo katika mwaka huu wa masomo.

Mambo ya Kuombea:

1.  Uinjilisti  –  Kila Mwanachama kuleta Roho moja kwa Kristo katika mwaka 
2017/18.
2.  Roho Mtakatifu na Mafanikio ya Global PCM Weekend
3.  Viongozi wa TUCASA katika ngazi zote.
4.  Umoja, Upendo na Ushirikiano katika TUCASA
5.  Mungu atusaidie tuweze kumpenda, kulipenda neno Lake na kipenda kazi yake.
6.  Mambo mengine kadri Bwana atakavyowaongoza

Comments

Popular posts from this blog

JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM SOMO LA TATU

JUMA LA MAOMBI LA VIJANA

MIKUTANO MIKUBWA YA INJILI INAENDELEA KATIKA ENEO LA VITONGA MLALI MOROGORO