JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM ALIHAMISI SOMO HILI NI MBARAKA SANA

Thursday, May 25, 2017SOMO: SIKU DUNIA ITAKAPOSIMAMA.Mwandaaji: Clinton Omuyanja, Mwenyekiti Msaidizi wa Union 




Fungu kuu: Yoshua 10:12,13. Mathayo 27:45-53.  Wimbo namba 107 kitabu kidogo.
Je, umewahi  kusikia dunia iliwahi  kusimama.  Wataalamu wa jiografia wanadai kuwa, 
dunia inapozunguka katika mhimili wake tunapata usiku na mchana. Dai hili si kweli kwa 
kuwa tangu mwanzo Mungu aliumba nuru na giza, nayo nuru ikatawala mchana na giza 
usiku [Mwanzo 1:4,5,16].
Ni kweli kuwa dunia imewahi kusimama zaidi ya mara moja katika historia. Dunia 
ilisimama wakati Yoshua akikabiliana na majeshi ya wafalme watano waliokwea dhidi 
yake na wana wa Israeli. Kwa ajili ya maombi ambayo Yoshua alimwomba Mungu, 
Dunia ilisimama kwa kuwa jua liliposimama haukuwa utaratibu wa kawaida kwa dunia.
Leo vijana tulioitwa na Kristo tunaitazama  dunia ambayo inaenda kwa mwendo 
unaoelezwa na Isaya 24:19 kuwa dunia inayumba yumba, yamkini tunaiona  kuwa 
mahali salama tukisahau miito yetu katika maombi na sala nakutenda kazi kwa kujitoa 
mioyo yetu katika shamba la Bwana.Ipo siku moja dunia itasimama.  
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017  TUCASA STUM
Tena  dunia ilisimama siku Yesu alipotoa sadaka ya uhai wake kwa ajili ya wanadamu 
wote. Siku hiyo aliposulubiwa, hatimaye alikata roho, mara dunia ikasimama kukawa na 
giza tangu saa sita hadi saa tisa. Ni takribani masaa matatu dunia ilishindwa kuvum ilia 
pale Kristo alipokata roho. Dunia haikustahimili kuwa katika namna yake ya kawaida.
Hapo dunia iliposimama nchi ilitetemeka, miamba ilipasuka, makaburi yakafunuka, na 
ikanuka miili ya wafu waliolala. Mathayo 27:45-53.
Ndipo tunapopewa tangazo kuwa iko siku dunia itakaposimama. Je ni siku ipi? Hakika 
ni siku Yesu atakaporudi, siku hiyo dunia itasimama tena. Matukio kama yale 
yaliyotokea wakati wa mauti ya Yesu yatatokea tena nayo  ni ufufuo wa wafu waliolala 
katika mavumbi ya nchi na haitaweza kusitahimili ujio huu wa Masihi.
Swali muhimu la kutafakari ni  hili, wakati dunia itakaposimama tutakuwa tukiendelea 
kuishi kwa namna inayotupendeza sisi wenyewe? Bila shaka kila mmoja wetu 
angetamani kuwa mmoja kati ya hao watakaomtukaza Mungu wakati dunia 
itakaposimama.  Wako wapi vijana watakao simama kumtetea Kristo wakati dunia 
inapoelekea Ukingoni? Ni akina nani watakao simama mahali pa Yoshua dunia 
inaposimama?
Ujumbe; Yeye aliyeiumba dunia na kuisimamisha wakati wa mauti yake atarudi tena na 
kuisimamisha dunia. Hivyo tunapaswa kusimama upande wake wakati Dunia 
inaposimama.
Wito: Tunaalikwa kujitoa kikamilifu  kwa Mungu, ili atujaze Roho wake huku tukifanywa 
tayari kuwa kama Yoshua aliyemtegemea Mungu hata ikawa alipoomba akasimamisha 
jua na dunia ikasimama. Ungana na  wana  TUCASA katika  union ya  kusini mwa 
Tanzania kuleta angalau roho moja kwa Kristo katika mwaka huu wa masomo.
Mambo ya Kuombea:
1.  Uinjilisti – Kila mwanachama kuleta roho moja kwa Kristo katika mwaka 2017/18.
2.  Roho Mtakatifu na mafanikio ya Global PCM Weekend
3.  Mfanikio ya SUMMIT ya  2018  –  Wahudumu, mahudhurio na Uongozi wa Bwana 
katika kila jambo.
4.  Kwaya za TUCASA  –  Mtindo wa maisha, mipango na roho ya uinjilisti iwe juu 
yao. 
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017  TUCASA STUM
5.  Machaplain na walezi wetu.
6.  Mambo mengine kadri Bwana atakavyowaongoza. 

Comments

Popular posts from this blog

JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM SOMO LA TATU

JUMA LA MAOMBI LA VIJANA

MIKUTANO MIKUBWA YA INJILI INAENDELEA KATIKA ENEO LA VITONGA MLALI MOROGORO