JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM

SOMO LA PILI 

Tuesday, May 23, 2017
SOMO: MTAZAMO, MSIMAMO NA MAONO YATAKAYO BADILI ULIMWENGU KWA
WAKATI KAMA HUU.
Mwandaaji: Karangi Joel, Mwenyekiti wa TUCASA ETC
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017  TUCASA STUM


Fungu kuu: Mwanzo 32:24-26.  Wimbo namba 107 kitabu kidogo.
Changamoto za sasa za kimaisha, kielimu, kiuchumi na kijamii wanazokumbana nazo 
vijana wakike na wakiume zimekua chachu kubwa kwa vijana kukata tamaa ya maisha 
na kurudi nyuma katika maisha yao ya kiroho. Mipango ya maisha ya baadae ambayo 
vijana  wamekuwa  wakijiwekea na ndoto ambazo wamekua wakizitazamia zitimie katika 
maisha yao zimekuwa  zikipotea pale tu changamoto zinapo wakabili nawao kushindwa 
kukabiliananazo.
Hali hii imewafanya vijana wengi hasa wanafunzi na wale wasio wanafunzi ambao 
wamekutana na nyakati tofauti kama hizi katika maisha kuchukua maamuzi yasiyo 
sahihi. Maamuzi hayo yamepelekea  kudumbukia katika dimbwi zito la kimaaamuzi, na 
maamuzi hayo kusababisha matokeo hasi katika maisha. Miongoni mwa hayo ni 
matumizi ya madawa ya kulevya, msongo wa mawazo na hata kujinyonga. Haya 
yamekuwa  ni matukio ya kawaida na  yakusikitisha kabisa yanayo kabili jamii ya vijana 
wanao mwamini Kristo na hata wale wasio amini.
Kijana Yakobo kwa muda  wa miaka 20, alikutana na chanagamoto nzito zilizompelekea 
kukaa katika njiapanda ya kimaamuzi.
1
Kuhusu kukwapua  baraka za kaka yake Esau 
na kuondoka kwa mjomba wake Labani pasipokuaga, akiwa katikati ya pori amekosa 
uelekeo,  ulikuwa  ni wakati muhimu wa kupima maamuzi sahihi ya Yakobo.  (Mwanzo
31:22, 23)
Katika dimbwi la kukata tamaa, dimbwi la upweke, dimbwi la kufeli ndio  wakati wa 
kusimama imara kama vijana kuyakita maisha yetu kwa Kristo. Kuyakabidhi maisha 
yetu kwake ndiyo njia pekee ya kuubadili ulimwengu katika nyanja zote za changamoto. 
Ndani ya hili juma la mibaraka na kujiweka wakfu hebu natung’ang’anie ulinzi wa Kristo 
pasipo kulegea.  (Mwanzo 4:24-26)  Maisha ya Yakobo kama kijana wa kipindi hicho 
yakawe chachu na mfano wa kusonga mbele katika kumtumaini Mungu na pia katika 
utumishi.
Pale Yakobo alipokuwa  na wasiwasi mkubwa juu ya hatima ya maisha yake, dhidi ya 
kaka yake Esau,  (Mwanzo 33:1)  na pale  mjomba wake Labani alipo mgeuka  (Mwanzo 
1
Spirit of Prophecy Vol.1 page 122-124 

Comments

Popular posts from this blog

JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM SOMO LA TATU

JUMA LA MAOMBI LA VIJANA

MIKUTANO MIKUBWA YA INJILI INAENDELEA KATIKA ENEO LA VITONGA MLALI MOROGORO