JUMA LA MAOMBI TUCASA STUM SOMO LA TATU
ENDELEA KUBALIKIWA
Wednesday, May 24, 2017
SOMO: UTUME NI WETU SOTE.
Mwandaaji: Maregesi January Simula, Mwenyekiti TUCASA SEC 2017/18
Fungu kuu: Mathayo 28:19, 20. Wimbo namba 107 kitabu kidogo.
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017 TUCASA STUM
matumaini katika mioyo yao lilikuwa limekuchwa, na giza ndilo liliwafunika.
Waliyakumbuka maneno ya Kristo wakiwa katika hali ya ukiwa na upweke kabisa.
Maneno ya Kristo yalisema hivi; “Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti
mbichi, itakuwaje katika mkavu?” Luka 23:31
Wanafunzi hali wakijawa na huzuni na majonzi wakiwaza sana kwamba ikiwa Yesu
waliyemwamini na kumtegemea amefanyiwa hivyo wao je, ni nini kitakachowapata
wao? Kwa hofu hiyo walikusanyika katika chumba cha juu, wakafunga milango,
wakiogopa wasipatwe na mambo yaliyompata Yesu. Hapa ndipo Mwokozi alipokutana
nao baada ya kufufuka kwake na kuwaambia maneno haya “Basi, enendeni,
mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana,
na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama,
mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.” Mathayo 28:19, 20
Agizo hilo lilikuwa limetolewa kwa wale wanafunzi kumi na wawili kwanza katika
chumba cha ghorofa, lakini sasa linatolewa kwa watu wengi zaidi hata kujumuisha na
kila Mwana TUCASA katika jimbo letu kuu la kusini mwa Tanzania. Wale wanafunzi
walipokuwa wakitafakari agizo hilo kwa hofu kubwa Yesu aliendelea kusema “Lakini
mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi
wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria na hata mwisho wa
nchi.” Matendo 01:08
Kristo aliwaagiza, wanafunzi wake wafanye kazi aliyowaachia tena kuanzia
Yerusalemu. Kazi ya wanafunzi ilikuwa lazima ianzie Yerusalemu. Kumbuka
Yerusalemu ndipo kilikuwa kitovu cha ibada zote za wayahudi hivyo wale waandishi,
mafarisayo, walimu wa dini na makuhani akina Kayafa waliokuwa wakimpinga Kristo
kwa nguvu kubwa walikuwa wenyeji wa Yerusalemu, ukiachilia mbali askari na utawala
wa kirumi kwa ujumla ambao pia ulikuwa kinyume na Kristo. Je, unaweza kuona kazi
kubwa waliyokuwa nayo wanafunzi wa Kristo kuanzia kazi ya utume Yerusalemu?
Wanafunzi wangeweza kuomba mahali pazuri zaidi pa kuanzia kazi, lakini hawakufanya
ombi kama hilo kwa Yesu.
Siku zote ili kuwa na matokeo makubwa zaidi ya kazi kuna maeneo mawili muhimu ya
kuanzia kazi hili pia lilifanyika kwa mitume wa Masihi.
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017 TUCASA STUM
1. Eneo la kwanza la kufanyia kazi ni maandalizi ya mtu binafsi kuingia kazini.
Hata wanafunzi wa Yesu walihitaji maandalizi binafsi ya kuingia kazini kwani hata wao
walikuwa hawajui nini hasa Yesu alikuja kukifanya duniani japokuwa alikaa nao miaka
mitatu na nusu katika utume, walikuwa bado hawajatambua kusudi la Yesu kwani hata
maswali yao yalionyesha hawakujua kusudi la Yesu kuja duniani, “Basi walipokutanika,
wakamwuliza, wakisema, Je, Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israel ufalme?
Matendo 1:06 “Yesu akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba
aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia
juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na
katika Uyahudi wote, na Samaria na hata mwisho wa nchi.” Matendo 01:7-8
Maandalizi ya mtu binafsi tunayopaswa kuyafanya ili kuingia kazini sio jambo lingine
bali ni yale maandalizi yaliyofanywa na mitume wakati wakingoja ahadi ya kupokea
nguvu ya Roho Mtakatifu. Ellen G. White anasema “Katika kutii agizo la Kristo,
[Wanafunzi] walisubiri katika Yerusalemi kwa ajili ya ahadi ya Baba ya umwagwaji wa
Roho. Hawakusubiri wakiwa wamekaa kizembe. Maandiko yanasema kuwa “Walikuwa
daima ndani ya hekalu wakimsifu Mungu” Luka 24:53. Kwa kadiri wanafunzi
walivyokuwa wakisubiri utimilisho wa ahadi walinyenyekeza mioyo yao katika toba ya
kweli, na kuungama dhambi ya kutokuamini kwao …. Wakiweka kando tofauti zao,
tamaa yote ya ukuu, walisogeleana karibu sana katika ushirika wa Kikristo” The Acts of
the Apostles uk. 3537 [1911] anaendelea kusema “Ilikuwa ni baada ya wanafunzi kuwa
wameingia katika umoja halisi, wakati ambapo hapakuwapo tena kushindania
madaraka ya nafasi ya juu kabisa, Ndipo Roho alipomwagwa.” Testimonies for the
Church, Vol 8 uk.20 [1904] na anasema tena “Tunapaswa kuomba kwa bidii kwa ajili ya
kushuka kwa Roho Mtakatifu kama wanafunzi walivyoomba katika siku ya Pentekoste.
Kama walimhitaji wakati huo, sisi tunamhitaji zaidi leo.” Testimonies for the Church, Vol
5 uk.158 [1882]
Kwa ufupi maandalizi hayo na zaidi tunapaswa sisi pia. Pale umoja wa dhati
utakapoonekana kati yetu Wana TUCASA kwa kumthamini kila mmoja wetu bila kujali
hali za kiuchumi, ngazi gani ya kielimu, kozi gani na umoja katika kila jambo
utakapoonekana, toba na maungamo ya dhambi za wazi na za siri yatakapofanywa,
tamaa yote ya mivuto ya kidunia katika chakula cha kidunia, mavazi ya kidunia,
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017 TUCASA STUM
kutohudhuria sherehe za kidunia, tamaa za ukuu (uongozi na madaraka), Usomaji wa
maandiko matakatifu utakapohuishwa ndani yetu, maombi ya dhati yatakapohuishwa
ndani yetu na mengine yanayofanana na hayo yatakapofanywa kwa dhati, ndipo
kuburudishwa kwa Roho kutakapoonekana ndani yetu ili tuingie kazini na matokeo ya
kazi yatakuwa zaidi ya enzi za mitume.
2. Anza kazi kwa mtu wa karibu yako kwanza.
Japo kuwa kuanzia kazi Yerusalemu lilikuwa ni jambo gumu kutokana na changamoto
tulizoziona hapo awali, Yesu aliagiza sharti kazi ianzie Yerusalemu, Desturi ya Injili
yenye mafanikio huanzia kwa mtu binafsi na hufuatia kwa mtu/watu wa karibu zaidi
kuliko wa mbali, tazama jambo hili kwa makini: - “Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa
amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake. Akamtazama Yesu akitembea,
akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu! Wale wanafunzi wawili wakamsikia
akinena, wakamfuata Yesu. Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia,
Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?
Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku
ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi. Andrea, nduguye Simoni Petro, alik uwa mmoja wa
wale waawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu. Huyo akamwona kwanza Simoni,
ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo).
Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana
wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).” Yohana 01:35 -42.
Tukio la Andrea kuonana na Yesu halikuwa jambo la kawaida, hili lilimfanya amwache
Yohana na kumfuata Yesu (Hatua ya kwanza imefanyika), wewe umeacha nini na
kumfuata Yesu? Alipokwisha kumfahamu Yesu mpaka mahali anapoishi alimwona
kwanza Simoni ndugu yake mwenyewe na kumwambia Tumemwona Masihi (Hatua ya
pili), Je, umemfahamu na umekutana na huyu Yesu katika maisha yako kiasi cha
kuanza kuwiwa kutangaza habari zake? Au Je, maisha yako yanadhihirisha wazi kuwa
umeonana na Yesu? Ndugu yako wa karibu wa pale chumbani kwako pale ‘Hostel’,
pale darasani kwako, pale katika kikundi chako cha ‘discussion’ nk Je umempasha
habari kuwa Umeonana na Yesu? Au mwenendo na matendo yanakusuta kusema
habari hizi za Yesu? Kwani hakuna utofauti kati yako na yeye kuwa ni nani aliyeonana
na Yesu? Zaidi ya kumwambia nduguyo, kifuatacho ni kumpeleka kwa Yesu kama
SOMO LA JUMA LA MAOMBI: MAY 21-27, 2017 TUCASA STUM
alivyofanya Andrea (Hatua ya tatu) naye ndugu yako ataitwa jina jipya kwake Yesu
yaani ataitwa Mwaadventista Msabato kama ilivyotokea kwa Simoni.
Witto: Wakati wimbo Na. 107 “Sauti ni yake Bwana.” ukiimbwa taratibu kwa sauti ya
chini kila mmoja ayatafakari maneno ya wimbo huo kwa kina huku mkazo wa kila
mmoja wetu kuingia shambani mwetu ukiendelea kutolewa.
Mambo ya Kuombea:
1. Uinjilisti – Kila mwanachama kuleta roho moja kwa Kristo katika mwaka 2017/18.
2. Roho Mtakatifu na mafanikio ya Global PCM Weekend
3. Familia zetu, wazazi na walezi.
4. Viongozi wa kanisa.
5. Wahitaji na wagonjwa.
6. Mambo mengine kadri Bwana atakavyowaongoza.
Comments
Post a Comment